Mfanya biashara agundulika akiwa amefariki Dunia Mkoani Singida
SINGIDA
Mfanyabiashara Tausi Hamisi @ Angel Edward, (39), Msubwa mkazi wa Ipembe – Manispaa ya Singida akutwa
akiwa amefariki Dunia pembeni mwa choo cha wanawake cha Hoteli ya KBH iliyopo
katika Maeneo ya KBH Hotel, Kata ya Mughanga, Tarafa ya Unyakumi Manispaa ya
Singida.
Akiongea na
waandishiwa wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishina
Msaidizi wa Polisi (ACP) Debora D. Magiligimba jana amaeleza kuwa tukio hili lilitokea siku
ya tarehe 24.08.2017 majira ya saa 11:30 alfajiri ambapo ameeleza kuwa Chanzo cha kifo hicho bado hakijajulikana
Kamanda
Magiligimba meeleza kuwa Jeshi la Polisi
limefanya uchunguzi wa awali wa tukio hilo na kubaini kuwa Mareheumu aliondoka
nyumbani kwao siku ya tarehe 23.08.2017 jioni na kuambatana na wenzake kwenda
katika ukumbi wa UHASIBU ambapo kulikuwa na harusi. Baadae usiku huohuo
walikwenda katika ukumbi wa Sky way Night Club kuendelea na starehe.
Hata hivyo
Kamanda ameeleza kuwa usiku huo huo walitoka
Sky way Night Club na kwenda Maeneo ya KBH Hotel akiambatana na rafiki yake
aitwaye Salima Mohamed, (28), Mkulima na mkazi wa Majengo – Manispaa ya Singida
na Mwanaume mwingine ambaye hakufahamika kwa Majina wala makazi ambapo
inasemekana waliendelea na starehe Hotelini hapo wakiwa watatu ambapo ilifikia
muda Marehemu akaenda kujisaidia ndipo Mwanaume waliyekuwa naye alimfuata na
hawakurudi tena hadi mlinzi alipogundua mwili wa Marehemu siku ya tarehe
24.08.2017 majira ya saa 11:00 alfajiri.
Kuhusiana na
tukio hilo ACP Magiligimba ameeleza kuwa
Jeshi la Polisi linawashikilia Watu wawili ambao ni Haruna Athuman, (34),
Mlinzi wa KBH Hoteli mkazi wa Kindai Manispaa ya Singida na Salima Mohamed,
(28), kwa mahojiano.
Kamanda
Magiligimba amesema Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya
Mkoa Singida kwa uchunguzi wa Daktari na
baada ya uchunguzi kuakamilika utakabidhiwa kwa ndugu kwa hatua za mazishi na
akatoa wito kwa Wananchi kubadilika na kuacha kuambatana na watu wasiowafahamu
katika maeneo ya starehe na pia inapotokea wawe wepesi wa kumdadisi mtu kujua
kama ni mtu mwema na wanapomtilia mashaka, watoe taarifa kwa Jeshi la Polisi
ili watu hao wakamatwe kabla hawajatekeleza vitendo vya uhalifu.
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
Komaa jamaa msetoperfecttz is under contruction bro
ReplyDelete