Idadi ya Watahiniwa wa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi Mkoa wa Singida yaongezeka kwa asilimia 35%
Idadi ya Watahiniwa
wa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi Mkoa wa Singida yaongezeka kwa asilimia 35%
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
Na. Sylvestare Richard
SINGIDA.
SINGIDA.
Idadi ya Watahiniwa
wa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi Mkoa wa Singida inayoanza leo imeongezeka
hadi kufikia wanafunzi 28,947 kutoka wanafunzi 21, 417 waliofanya mitihani hiyo
hiyo mwaka jana.
Ongezeko hilo la
wanafunzi 7,530 ni kiashiria cha kuboreshwa kwa elimu na usimamizi wa sekta ya
elimu msingi kwa Mkoa wa Singida pamoja na jitihada za wazazi na walezi kuhakikisha
wanafunzi wanahudhuria masomo yao ipasavyo.
Hayo yamebainishwa jana na Afisa Elimu Mkoa wa Singida Florian Kimolo ambaye amefafanua kuwa jumla
ya wasichana 15,964 na wavulana 12,984 wameungana na wenzao Nchi nzima kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya darasa la saba hapo jana kwa kuanza kufanya mtihani wa Kiingereza ukifuatiwa na mtihani wa Hisabati.
Kimolo ameeleza kuwa
ongezo la wanafunzi wanaofanya mitihani inaweza kusababishwa na idadi kubwa ya
udahili wa wanafunzi hao kwa mwaka walioanza darasa la kwanza, lakini pia sababu
nyingine kubwa ni usimamizi mzuri katika sekta hiyo ambao umepunguza utoro wa wanafunzi
uliokuwa ukipelekea wanafunzi hao kuacha shule.
Amefafanua kuwa wanafunzi
wanaweza kudahiliwa wengi lakini wakamaliza wachache kutokana na sababu
mbalimbali ikiwemo utoro, kuacha shule, uhamisho, na vifo hivyo idadi
ya watahiniwa inapoongezeka ni ishara kuwa walimu, wazazi/walezi na idara za
elimu ngazi zote zimefanya kazi nzuri ya kusimamia sekta hiyo.
Kimolo amesema
mitihani imeanza kufanyika kwa amani na utulivu kutokana na kuwa ofisi yake imefanya
maadalizi mapema kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na halmashauri zote za
Mkoa wa Singida.
Aidha amewataka
wasimamizi kuzingatia maadili, kanuni na sheria walizoelekezwa wakati wa semina
za usimamizi ili mitihani ifanyike kwa haki bila ya matatizo yoyote.
Kimolo ameongeza kuwa
jumla ya vituo vya kufanyia mitihani hiyo kwa mkoa wa Singida ni 518 huku
mikondo ikiwa 1313 huku akiwasisitiza wanafunzi hao kufanya mitihani kwa amani
na nidhamu.
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
No comments