Watu wawili wadhaniwa kufariki dunia baada ya kufukiwa na mgodi Mkoani Singida
Watu wawili wadhaniwa kufariki
dunia baada ya kufukiwa na mgodi Mkoani Singida.
Na Sylvester Richard.SINGIDA
Watu wawili wanadhaniwa kufariki Dunia Mkoani Singida baada ya kufukiwa na udongo wa Mgodi wakati wakichimba madini.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake hii leo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Mrakibu mwandamizi (SSP) Isaya K. Mbughi ameeleza kuwa tukio hilo lilitoke siku ya
tarehe 09.09.2017 majira ya saa 7:47 usiku katika Kijiji cha Konkilangi,
Kata ya Ntwike, Tarafa ya Shelui, Wilaya ya Iramba katika Mgodi
ujulikanao kwa jina la Sekenke 1 katika kitalu namba 1 ambapo maduara matano yanayomilikiwa
na Marijan Ramadhani na Jakobo Ntobi yalititia na kusababisha majeruhi kwa
wachimbaji 5 ambao waliwahi kuokolewa na wengine wawili wanadhaniwa kufariki
dunia wakati juhudi za kuopoa miili yao zikiendelea.
Kaimu Kamanda amewataja Waliojeruhiwa
katika ajali hiyo ambao tayari wameokolewa kuwa ni pamoja na; Ayubu
Msengi, (34), mnyiramba, mkazi wa Ntwike ana jeraha kichwani na maumivu
kiunoni, Mwita Salumu, (42), mnyiramba, mkazi wa Gumanga ana maumivu bega la
kushoto na ubavu wa kushoto na Lazaro Edward, (28), mnyiramba, mkazi na mkulima
wa Kiomboi Soweto ambaye anajeraha kichwani na maumivu shingoni.
Aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Jeremi Idd,
(41),mnyiramba, mkazi wa Kijiji cha Gumanga anamaumivu kiunoni na Jumanne Said,
(24), mnyiramba na mkazi wa Mgongo anamaumivu kichwani na kusema hali zao
zinaendelea vizuri baada ya kupata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Iramba.
Hata
hivyo SSP Mbughi amewataja wachimbaji wawili ambao ni Simon Odochi,@ Wa Mwanza,
anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 26, Mkurya, na mkazi wa Mwanza na Kashinde Nkula
anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 27, mkazi wa Kijiji cha Mangasu, Wilaya ya
Kishapu Mkoani Shinyanga, wote wachimbaji wadogo wa madini wanaosadikiwa kufariki dunia wakiwa bado
wamefukiwa na kifusi ambapo Jeshi la Polisi kwa kusaidiana na wananchi linaendelea
na juhudi za kuopoa miili yao kwa kutumia vifaa mbalimbali likiwemo gari
maalumu (CATAPILLER).
SSP Mbughi ameeleza kuwa Jeshi
la Polisi kwa kushirikiana na wataalam wa Migodi wanaendelea na uchunguzi ili
kubaini chanzo hasa cha kutitia kwa migodi hiyo
Kaimu kamanda ametoa wito kwa wamiliki wa Migodi kuzingatia sheria
za usalama wa Migodi. Pia ameatoa wito kwa mamlaka za ukaguzi wa Migodi kufanya
ukaguzi wa mara kwa mara ili kuepusha ajali zisizo za lazima na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi linawatafuta wamiliki wa Mgodi huo waliotoroka baada ya ajali hiyo.
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
No comments