Mtu mmoja ashikiliwa na Polisi Mkoani Singida kwa kupatikana na Mirungi na wengine wawili kwa kuuza petroli kinyume cha sheria.
WATU WATATU WASHIKILIWA MKOANI SINGIDA KWA MAKOSA MAWILI TOFAUTI
SINGIDA.
Jeshi la Polisi
Mkoani Singida linawashikilia watu watatu kutokana na matukio mawili
yaliyojitokeza semu na nyakati tofauti.
Akiongea na
waandishi wa habari hivi jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida
Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP)
Debora D. Magiligimba ameeleza kuwa
tukio la kwanza ni tukio la ukamatwaji wa mtuhumiwa anayejihusisha biashara ya
dawa za kulevya ain ya mirungi aitwaye Haji Yahaya, (28), Muha, Dereva na Mkazi
wa Mwanza.
Kamanda
Magiligimba amaeeleza kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na Askari wa Jeshi la
Polisi siku ya tarehe 21. 08. 2017 majira ya saa 8:00 mchana akiwa kwenye gari
Na. T.250 BEQ BUS mali ya Kampuni ya ABOOD akitokea Mwanza kwenda Dar es salaam
ambapo Jeshi la Polisi lilipata taarifa hizo ndipo Basi hilo lilipofika Mkoani
Singida lilikamatwa na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Singida na kufanyiwa
upekuzi ambapo katika upekuzi huo lilipatikana begi la Mtuhumiwa lililokuwa na
mirungi bunda 24 ambayo ni sawa na Kg. 12 ndani yake likiwa limehifadhiwa
kwenye buti.
Aidha ACP
Magiligimba amaesema kuwa Mtuhimwa
anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano ili kufahamu mtandao wote
anaoshirikiana nao katika biashara hiyo ili nao wakamatwe na kufikishwa
mahakamani. Kamnda amechukua nafasi hiyo pia kuwataka wananchi wote wa Mkoa wa
Singida na Nchi kwa ujumla kuachana na
biashara ya dawa za kulevya ambayo ni kinyume cha sheria za Nchi. Jeshi la
Polisi Mkoa wa Singida linaendelea na misako mbalimbali ya kubaini mitandao
inayojihusisha na dawa za kulevya na uhalifu mwengine wenye dalili ya kuvunja
amani ya Nchi.
Katika tukio la
pili ACP Magiligimba ameeleza kuwa ni tukio la kuungua moto kwa nyumba ya
Asheri James,(67) Mnyiramba, Mkulima na mkazi wa Veta – Stesheni ambapo ameeleza
kuwa katika ajali hiyo ambayo ilitokea siku ya tarehe 22.08.2017 majira ya saa
2:15 usiku watu wawili ambao ni Rashid Omari, (45), na
Hawa Shabani, (32), wanandoa na wapangaji
katika nyumba hiyo wameungua sehemu mbalimbali za miili yao.
Magiligimba
ametanabaisha kuwa chanzo cha moto huo ni dumu lililokuwa na mafuta ya petrol
kushika moto na kwamba wanandoa hao wana duka lao katika nyumba hiyo ambamo
wanauza bidhaa mchanganyiko ikiwemo mafuta ya petrol ambapo siku ya tukio
alifika mteja akihitaji petrol Lita moja na kuhudumiwa na Hawa Shabani hivyo wakati akirudisha dumu lililokuwa na Petrol ndani likiwa halijafunikwa alilipitisha
karibu na mshumaa uliokuwa ukiwaka ndipo moto ulipolipuka na kuliunguza dumu
hilo na moto kushika nguo za Hawa
Shabani na kuungua zote. Katika harakati za kumwokoa Mke wake Rashid Omari naye aliungua kisha moto
kusambaa katika vyumba vingine.
Ameeleza kuwa kuhusiana
ajali hiyo Jeshi la Polisi linawashikilia wanandoa hao huku wakiendelea
kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa Singida kwa kosa la kufanya biahsara
ya Petrol mahali ambapo siyo halali kwa biashara hiyo.
ACP Magiligimba ametoa wito kwa
wafanyabiashara wote kuacha kufanya biashara ya petrol na nishati zingine
zinazofanana na hizo katika maeneo yasiyo rasmi kwa biashara hizo ili kuepukana na majanga ya moto yanayosababishwa
na nishati hizo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida
Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP)
Debora D. Magiligimba akionesha mabunda ya Mirungi kwa waandishi wa habari Ofisini kwake.
Pichani ni Mabunda ya Dawa za kulevya aina ya Mirungi yaliyokamatwa Mkoani singida.
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
No comments