Watu sita wamefariki Dunia Mkoani Singida na wengine 22 kujeruhiwa baada Gari walilokuwa wakisafiria kupinduka.
Watu sita wamefariki Dunia Mkoani Singida na wengine 22 kujeruhiwa baada Gari walilokuwa wakisafiria kupinduka.
Watu sita wamefariki Dunia Mkoani Singida na wengine 22 kujeruhiwa baada Gari lenye
namba za usajili T.806 AEL SCANIA lori mali ya Abdalla Mussa, (39), Mnyaturu,
Mfanyabiashara na Mkazi wa Mwenge Singida, likiendeshwa na Dereva aliyekimbia
baada ya ajali hiyo anayefahamika kwa jina la Juma Jumanne @ Kidanka, (32), Mnyaturu,
na mkazi wa Mnung’una-Singida likitokea Mtinko kwenda Singida kupinduka.
Akiongea na waandishi wa habari Ofisini kweke hii leo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora D. Magiligimba ameeleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 1:30 usiku huko katika Kijiji na Kata ya
Kijota, Tarafa ya Mtinko, Wilaya Singida barabara ya
Mtinko – Ilongero,
Amewataja waliofariki
katika ajali hiyo kuwa ni pamoja na Haji
Jumanne, Mnyaturu, umri kati ya miaka 28-35, mkazi wa Mrama, Mikidadi Mohamed, Mnyaturu, umri kati ya miaka
35-40, Mkazi wa Ilongero na Musa salim,
Mnyaturu, umri kati ya miaka 35-40, mkazi wa Mwakiti.
Wengine
ni Allen Mwangu, Mnyaturu, umri kati ya miaka 30-38, mkazi wa
Ikungi, Lucas Stephano, mnyaturu, miaka 40, mkazi wa
mlama na Sharifa Omari, mnyaturu, miaka 19, mkazi wa Ilongero
wilaya ya Singida vijijini.
Aidha Kamanda amewataja
waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Fadhili Jumanne , (33), Mnyaturu, Mkazi wa Kibaoni - Singida, Mikidad
Hamisi, Jafari Hamis, na Idrisa Ibrahimu, ambao wote wamevunjika miguu na
kulazwa katika Hospitali ya Hydom, Mkoani Manyara na hali zao siyo nzuri.
Wengine
ni Samwaga Hango, (26) Mnyaturu, Mkazi wa Singida Mjini, amevunjika mguu wa
kushoto, Hamza Hassani, (24), Mnyaturu, Mkazi wa Singida Mjini amevunjika mguu,
Mwajuma Rajabu , (45) Mnyaturu, Mkazi wa Ilongero amepasuka bandama pamoja na
majeruhi wengine 10 wamepata maumivu sehemu mbalimbali za miili yao na wamelazwa katika Hospitali ya Misheni Mtinko.
Majeruhi
wengine ni Asha ramadhani, (42), Mnyaturu, Francisca John, (43), Muhango,
Mariamu Juma, (50), Mhango wote wakazi wa Irongero ambao wamelazwa katika
Hospitali ya Ilongero na Nuru said (19), Mnyaturu, Mkazi wa Ilongero,
amevunjika paja la kushoto na maumivu Mkono wa kulia, Ally Ibrahim, (21), mnyaturu,Mkazi wa
Ilongero ambao amevunjika mguu wa kulia na wote wamelazwa katika hospitali ya
Mkoa wa Singida na hali zao siyo nzuri.
Ametaja Chanzo
cha ajali hiyo kuwa ni uzembe wa Dereva kutokuwa makini akiwa anaendesha gari hilo barabarani pamoja na
kupakia mzigo kwa njia ya hatari.
Hata
hivyo uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa kabla ya ajali hiyo
siku ya tarehe 12.08.2017 Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa wa Singida SP Peter
Majira alifanya kikao na wamiliki wa magari ya mizigo akiwepo Mmiliki wa Gari
iliyopata ajali ambapo alitoa elimu juu ya matumizi sahihi ya magari ya mizigo.
Hata hivyo pamoja na elimu hiyo kutolewa, Mmiliki wa gari Abdala Mussa alikaidi
maelekezo hayo na kupelekea ajali hiyo kutokea.
Kuhusiana
na ajali hiyo, Jeshi la Polisi linamshikilia Mmiliki wa Gari kwa mahajiano na
baada ya mahojiano kukamilika atafikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo
wake na Juhudi za kumtafuta dereva aliyesababisha ajali hiyo zinaendelea.
ACP Magiligimba hakusita kutoa wito kwa wamiliki wa vyombo vya moto
kusimamia vema matumizi sahihi ya magari yao
kulingana na sheria na taratibu za usalama barabarani na kuongeza kuwa Endapo gari imesajiliwa
kwa matumizi ya kubeba mizigo, itumike kwa kubeba mizigo na siyo kuchanganya
mizigo na Abiria na kama gari imesajiriwa kwa
matumizi ya kubeba abiria, itumike kubeba abiria siyo kuchanganya Abiria na
mizigo.
Kamanda Magiligimba hakuacha kutoa wito kwa a wito kwa wananchi/abiria kwa kuwaasa kuacha tabia ya kupanda katika magari ya
mizigo kwani kufanya hivyo ni kinyume na sheria, kanuni na taratibu za usalama
barabarani
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
sana kaka
ReplyDelete