Jeshi la Polisi lakanusha taarifa za Askari wa Jeshi la Polisi kuhusishwa na muendelezo wa tukio la kujeruhiwa kwa risasi kwa Mhe. Tundu Lissu (MB).
Jeshi la Polisi lakanusha taarifa za Askari wa Jeshi la Polisi kuhusishwa na muendelezo wa tukio la kujeruhiwa kwa risasi kwa Mhe. Tundu Lissu (MB).
Katika siku za karibuni kumejitokeza vitendo vya baadhi ya watu
kutumia majina ama picha za watu na kuwahusisha na matukio ya kihalifu
au matukio yanayohusiana na uhalifu kwa lengo la kujipatia umaarufu,
kuwachafua watu hao au kuwakosanisha na jamii inayowazunguka.
Kutokana na vitendo hivyo ACP Barnabas David Mwakalukwa ambaye ni Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu emekutana na Waandishi wa Habari na kueleeza kuwa Mnamo
tarehe 11.09.2017 kupitia mitandao ya kijamii kulisambaa picha ya askari
wa Jeshi la Polisi akihusishwa na muendelezo wa tukio la kujeruhiwa kwa
risasi kwa Mhe. Tundu Lissu (MB) ambapo taarifa hiyo ilimtambulisha
askari huyo kuwa ni kachero wa Kitengo cha Interpol na kwamba yupo
jijini Nairobi nchini Kenya akifuatilia taarifa za Mhe. Lissu.
ACP Mwakalukwa ameeleza kuwa Jeshi
la Polisi linapenda kukanusha taarifa hizo kuwa si za kweli na ni za
uongo zenye lengo la kumchafua askari huyo na Jeshi la Polisi kwa
ujumla na kuongeza kuwa Askari huyo hayupo Nairobi kama ilivyoenezwa na picha
iliyotumika ilipigwa hapa nchini tarehe 07.01.2017 kwenye sherehe ya
mahafali ya mtoto wa kaka yake.
Akiongea Kuhusiana na safari ya Nairobi, ACP Mwakalukwa amesema
askari huyo alikuwa Nchini Kenya kwa kozi ya kimafunzo kuanzia tarehe
04.09.2017 na kurejea tarehe 08.09.2017, huku Mhe. Lissu akipatwa na
mkasa wa kujeruhiwa kwa risasi Tarehe 07.09.2017 na kusafirishwa kwenda
Nairobi usiku wa kuamkia tarehe 08.09.2017.
Aidha Mwakalukwa amesisitiza na kusema kuwa Jeshi la Polisi linakemea
vikali kitendo hiki chenye lengo la kumharibia maisha yake askari huyo,
na linawataka wale wote waliohusika kusambaza au kutajwa katika taarifa
hizo kuripoti kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa
ajili ya mahojiano na kutoa onyo kwa wote wanaofikiri kuwa
wanaweza kukaa na kupika habari ili waweze kuivuta jamii iwe upande wao
na kuchafua upande wa serikali.
Akizungumzia suala la Mhe. Lissu ameeleza kuwa lipo chini
ya uchunguzi ili kuwabaini wote waliohusika na tukio hili na hatimaye
kuwafikisha mahakamani na kuwataka wananchi na wanasiasa wakaliacha Jeshi
la Polisi liweze kufanya kazi yake bila kuliingilia ili kuweza kupata
ukweli wa jambo hili.
Hata hivyo ACP Mwakalukwa ameitaka Jamii itambue kuwa Jeshi la Polisi
linafanyakazi kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu za Nchi na kamwe
halifanyi kazi kwa kuvizia na kueleza kuwa endapo mtu yeyote anahitaji taarifa, Jeshi la Polisi lina mifumo rasmi inayoliwezesha kupata taarifa linazozitaka kupitia
uhusiano uliopo ndani na nje ya Nchi na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi kupitia
Kitengo cha upelelezi wa makosi ya mitandao (Cyber Crime Investigation
Unit) linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wote waliohusika na
kusambaa kwa taarifa hizi za uongo ili hatua za kisheria zichukuliwe
dhidi yao.
Mwakalukwa ametoa rai kwa wananchi kuacha kutumia
mitandao ya kijamii vibaya na badala yake mitandao hii itumike kwa ajili
ya kuelimisha na kuihabarisha jamii juu ya masuala mbalimbali ya
kimaendeleo.
Kama una Habari., Matangazo, Picha, Maoni na
ushauri , tuma kupitia anwani zifuatazo;
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
E-mail sylvestermac87@gmail.com/machibya.richard@yahoo.com
Sim no . 0768367454/0652683063 . WhatsApp 0629655814
No comments